Hakimu
Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Thomas Simba ameagiza
aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, afike Mahakamani
kesi yake itakapotajwa tena mnamo Disemba 19 Mwaka huu baada ya
Mdhamini wake kutoa uthibitisho wa Maendeleo ya Lissu Mahakamani.
Alipokuwa akitoa uthibitisho huo Mdhamini wa Lissu, Ibrahim Mohamed
aliieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Lissu amepona lakini
amesema hawezi kurudi Nchini kwa sababu ya kuhofia usalama wake.
Hakimu
Simba alimkatisha na kumueleza kuwa; "Sisi hatutaki siasa hapa, namtaka
Mshtakiwa, naahirisha kesi hadi December 19,mwaka huu siku hiyo nataka
Lissu awepo."
Mbali na Lissu washtakiwa wengine ni, wahariri Simon Mkina, Jabir Idrisa na mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehbooh.
Kwa
pamoja washtakiwa hao, wanakabiliwa na mashtaka matano ikiwamo kuandika
habari za uchochezi kinyume na Sheria ya Magazeti ya mwaka 2002.
Ilidaiwa
kuwa kati ya Januari 12 hadi 14, 2016 jijini Dar es Salaam, washtakiwa
Jabir, Mkina na Lissu, waliandika na kuchapisha taarifa za uchochezi
zenye kichwa cha habari kisemacho, 'Machafuko yaja Zanzibar.'