SADC KUWA NA VISA MOJA KUPUNGUZA URASIMU



Ahmed Mahmoud/Arusha

Naibu Katibu Mtendaji Mkuu wa Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) Thembinkosi Mhilongo amesema umoja huo umedhamiria kuwa na VISA moja kwa lengo la kupunguza urasimu ndani ya Jumuiya hiyo
Image result for Dkt Thembinkosi Mhlongo
Hayo yameelezwa leo na Naibu Katibu Mtendaji Mkuu wa SADC Dkt Thembinkosi Mhilongo wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wenye dhamana na Wizara za Mazingira,Maliasili  na Utalii katika nchi hizo za Ukanda wa Kusini mwa bara la Afrika (SADC).

Dkt Mhilongo pia amesema nchi za SADC zimejipanga  kuangalia kwa kina   suala la Viumbe na Mimea vamizi katika nchi  hizi wanachama  pamoja na Wanyama ambao wako katika hatari ya kutoweka katika nchi hizo.

Naibu Mtendaji Mkuu huyo wa SADC amewataka Mawaziri  hao wenye dhamana ya mazingira, maliasili na utalii kuhakikisha  wanaangalia kwa kina Itifaki na Mikataba  inayohusu Sekta hizo tatu katika nchi Wanachama za SADC 

Amesema Mkutano wa Mawaziri hao ni muhimu katika kukuza na kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa mataifa ya SADC hivyo amewataka wakati wa Mkutano huo kupima na kuangalia kwa kina  Sera na Itifaki zinazosimamia  Sekta hizo tatu ambazo ndio muhimili mkuu wa Uchumi wa mataifa hayo.

Mbali na kuangalia masuala hayo Naibu Mtendaji Mkuu huyo wa SADC amewataka Mawaziri hao kuhakikisha wanaangalia  kwa Kina Sheria zote zinazosimamia  na kuongoza Sekta hizo katika Jumuiya.


Amesisitiza kuangaliwa upya Itifaki ya Utalii, Mazingira, na Maasili katika nchi Wanachama za SADC na mabadiliko ya tabia nchi pamoja na umuhimu kwa Mawaziri hao kuhakikisha majandiliano ya Mkutano wao yanalenga katika kutatua changamoto zinazokabili sekta ya mazingira, maliasili na Utalii katika nchi za SADC


Nchi za SADC imebahatika kuwa na raslimali  lukuki zikiwemo za Wanyamapori, misitu, Uvuvi  rasilimali ambazo  ni muhimu katika kuchangia ukuaji wa Uchumi na maendeleo ya  nchi wanachama za SADC.


Amewataka Mawaziri hao kuangalia kwa kinja Itifaki  ya SADC  inayohusu umuhimu wa kusimamia na kulinda uhifadhi, kuangalia Itifaki ya misitu, Uvuvi na  Sheria ya usimamizi wa Wanyamapori

Pia amesisitiza umuhimu kwa SADC Kutambua umuhimu wa kusimamia , kulinda na kuhifadhi misitu ili kuwa na uhifadhi endelevu katika nchi hizi za Ukanda wa Kusini mwa Afrika

Naibu Mtendaji Mkuu huyo amesema Jiji na Mkoa wa Arusha limebeba  historia  kubwa ya SADC kutokana na kuwa Jiji hili ndipo chimbo kubwa la kuanzishwa kwa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini Mwa Afrika miaka 40 iliyopita

Amesema SADC iliasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Mzee Keneth Kaunda wa Zambia, Rais Somora Machel wa Msumbiji, Rais Agustino Neto wa Angola na Rais Gabriel Mugabe wa Zimbabwe ambapo Jumuiya hiyo iliasisiwa katika Ukumbi huo wa AICC

Aidha Mkataba wake ulisainiwa Lusaka Nchini Zambia  kwa ajili ya kuanzishwa kwa Jumuiya hiyo ambapo Makao ya SADC yapo Gaboro Nchini Botswana

Kukosekana kwa Visa moja  kwa Watalii  ulaya wanapokuja  katika ukanda huu wa kusini mwa nchi za kusini mwa Afrika ni moja ya changamoto kubwa

This is received, thanks for your comments, will come back to you

Previous Post Next Post