Na Mwandishi Wetu, Dar es salaam
Kampeni ya Mnada kwa Mnada imeanza 0ktoba 11 katika
maeneo Kome Pamoja Maisome kwa siku mbilimbili ikiwa ni kuwafikia
wananchi wengi katika wilaya hiyo.
Akizungumza
katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada katika Viwanja vya Nyehunge Wilayani
Sengerema Mkuu wa Kanda Ziwa Mhandisi Francis Mihayo amesema
wamejipanga kuwafikia wananchi wote wawemejisajili laini za simu kwa
alama za vidole.
Wananchi wakipata huduma ya Usajili wa Vitambulisho vya Taifa katika Viwanja Nyahunge |
Mhandisi Francis Mihayo akizungumza na wananchi wakati wa Kampeni ya Mnada kwa Mnada uliofanyika katika Viwanja vya Nyehunge Sengerema |
Wananchi wakisoma vitabu vya muongozo wa TCRA katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada Nyehunge Sengerema. |
Kampeni
tangu imeanzishwa imekwenda katika Mikoa 16 lengo kuu ni nchi nzima
kufiwa na Kampeni hiyo katika kuwawezesha wananchi kupata elimu ya
Mawasiliano Pamoja usajili wa laini za simu kwa alama za vidole.
Amesema
ni fursa kwa wananchi wa Sengerema kujitokeza kujisajili laini za simu
kwa alama za vidole na huduma nyinginezo kutokana na kuwepo kwa
mnyororo wadau wa mawasiliano.
Aidha
Mihayo amesema kuwa Mnada kwa Mnada TCRA ilianzisha ili kutoa fursa
ya Wananchi kuhudumiwa hasa wakati huu usajili wa laini za simu kwa
alama za vidole ili wasiweze kumuacha mtu yeyote kutotumia simu ifikapo
Desemba 31 mwaka huu.
Amesema
muda uliopo ni miezi mitatu hivyo Wananchi wakamilishe taarifa
zinazohitajika katika kujisajili laini za simu kwa alama za vidole ili
kuondoa usumbufu mwisho wa Desemba kwa watu kupanga foleni.
Mhandisi
Mihayo amesema Kampeni hiyo ni kuimarisha ulinzi katika mawasiliano ya
simu pamoja kufanya mawasiliano kuwa salama katika nchi.
Amesema
kuwa kampeni ya Mnada kwa Mnada ni kwa ajili ya kutoa elimu ya
mawasiliano kwa kushirikiana na wadau katika kujibu changamoto
wanazokutanazo katika utumiaji wa mawasiliano nchini.
Amesema
kuna watu wengine wanatumia mawasiliano ya simu bila kujua ambapo Jeshi
Polisi lipo katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada ili kuwaelewesha makosa
ya jinai ya matumizi ya simu.
Aidha amesema Kampeni
hiyo ni endelevu katika kuwafikia ikiwa kuhakikisha kila mwananchi
anajisajili laini yake kwa alama za vidole kwa kutumia kitambulisho cha
taifa cha NIDA.
Mhandisi
Mihayo amesema kuwa TCRA iko kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi ili
mtumie Mawasiliano kwa usalama kutokana na elimu tunayotoa.
"TCRA
tupo tayari kuwafikia wananchi katika utoaji wa elimu za utumiaji wa
bidhaa za mawasiliano kwa kutatua changamoto katika huduma hiyo" amesema
Mhandisi Mihayo.
Nae
Afisa Mawasiliano Mwandamizi wa TCRA Mabel Masasi amesema kuwa mwitikio
umekuwa mkubwa kwa Wananchi kutaka vitambulisho kwa ajili ya kusajili
laini za simu kwa alama za vidole hali na kufanya wananchi wengi
wamepata vitambulisho vya Taifa na kusajili laini za simu kwa alama za
vidole.
Masasi amesema
Wananchi wa watumie Kampeni ya Mnada kwa Mnada ya TCRA kupata elimu na
baada ya kuisha Mnada sehemu husika waende katika mamlaka husika kupata
vitambulisho.
Ameongeza kuwa watahakikisha kila mwananchi anajisajili kwa alama za vidole kwani Watu wana haki ya kuwa na mawasiliano ya simu