Watumia machela za miti kupeleka wagonjwa hospital, watembea umbali wa km32

<
Na Mwandishi Wetu, NJOMBE

Wakazi wa kijiji cha Kitewele kilichopo mwambao mwa ziwa Nyasa chenye jamii za wafugaji,Wavuvi na Wakulima wilayani Ludewa Mkoani Njombe wanalazimika kusafirisha wagonjwa kwa machera za fimbo za miti na mhanzi umbali wa zaidi ya km 32 ili kunusuru maisha ya ndugu zao,Hatua inayosababishwa na uwepo wa barabara ambayo haipitiki kwa gari ama chombo cha moto.

Barabara hiyo inayounganisha vijiji vya Madunda,Kitewele na Nakonde ilichimbwa miaka michache iliyopita kwa mkono na wakazi wa kijiji cha Kitewele chenye wakazi zaidi ya elfu moja huku lengo kuu likiwa ni kufungua mawasiliano ambayo yaliwafanya kuishi kama watu waliojitenga.

Wakipaza sauti katika mkutano wa mbunge wa Ludewa wenye lengo la kusikiliza kero za wananchi akiwemo Beno Lwiva na Kasilida Haule wanasema katika kijiji chao kuna zahanati lakini haifikiki vyombo vya moto hivyo endapo mgonjwa analetwa ama kupata rufaa hulazimika kutengeneza machera za miti na kisha kutembea umbali mrefu  hali ambayo inasababisha baadhi yao kupoteza maisha wakiwa njiani hivyo wanaomba serikali ione umuhimu wa kuunga mkono jitihada walizofanya kwa kurekebisha barabara hiyo.

Mbali na ubovu wa barabara kuhatarisha uahai wa wagonjwa lakini pia wakazi hawa wanasema imeathiri kwa kiasi kikubwa uchumi wa kijiji hicho kwani soko la mazao limekufa kabisa.

"Ndugu zetu wengi wanapoteza maisha kwasababu ya ubovu wa barabara hii,tunabeba kwenye machera za miti ya mihanzi kupeleka wapendwa wetu hospitali ya Wilaya Luddewa na Milo hivyo tunaomba mtusaidie mh Mbunge" Alisema Beno Lwiva 

Ukitolewa Ufafanuzi juu ya hatua zinazokwenda kuchukuliwa ili kumaliza adha hiyo na kunusuru maisha ya wagonjwa,kilimo na sekta ya biashara katika ukanda huo Meneja wa TARURA wilaya ya Ludewa Enhad Willa amesema tayari ameitazama barabara hiyo na kuelewa maeneo yote korofi hivyo ili iweze kukarabatiwa inapaswa kusajiliwa kwenye barabara za tarura ndipo mwaka ujao itengewe bajeti ya kutosha 

Nae mbunge wa Ludewa Mbunge Joseph Kamonga wakati akieleza anachokwenda kufanya ili kumaliza kero alizopokea ikiwemo ya pembejeo,umeme,barabara,elimu na afya akasema anakwenda kuanza na kutoa bati 40 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya kisasa ya mwalimu katika shule ya msingi Kitewele huku suala la barabara akitaka tarura ilipe uzito mkubwa .

Kuhusu bei ya mazao na pembejeo Kamonga akasema tayari suala hilo amelisemea bungeni limeanza kupatiwa ufumbuzi kwa serikali kuanza kununua mahindi kwa wakulima na kisha kuanza ujenzi wa kiwanda cha mbolea mkoani Dodoma.

"Ninachokiomba kwenu tarura suala la barabara hii ya Madunda,Kitewele na Makonde ifanyiwe kila jitihada ikamilike kwani wananchi wanateseka sana hapa ,haiwezekani kijiji kina wakazi zaidi ya elfu 1 kikose barabara ya uhakika .

This is received, thanks for your comments, will come back to you

Previous Post Next Post