Na Moshi Ndugulile
Wajumbe wa Mkutano Mkuu Umoja
wa wanawake wa CCM, UWT Wilaya ya Shinyanga Mjini, wamemchagua Bi Mariam kajala
kuwa mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Wilaya kupitia uchaguzi mdogo wa kuziba nafasi iliyokuwa wazi
Akitangaza matokeo hayo msimamizi Mkuu wa Uchaguzi huo Mjumbe wa
Baraza la UWT Taifa Christina Gule amemtaja Bi kajala kuwa mshindi wa nafasi
hiyo baada ya kupata kura 32 kati ya 54
akiwaongoza wagombea wengine watatu
Gule amewatangaza wagombea wengine waliokuwa wakiwania nafasi hiyo kuwa ni pamoja na Mery Izengo ambaye amepata kura 22,Mary Nzuku hakupata kura,na Theonestina Martine ambaye pia hakupata kura yoyote
Baada ya kutangaza matokeo hayo msimamizi Mkuu wa Uchaguzi huo Mjumbe wa Baraza la UWT Taifa Bi Christina Gule amemtaka kiongozi aliyechaguliwa Bi Mariam kajala kuitumikia kwa uadilifu nafasi hiyo,na kuhakikisha anakuwa kiungo na chachu ya kuchochea ushirikiano,umoja na mshikamano baina ya Wanachama na viongozi wa Chama na jumuiya zake.
Akizungumza baada ya kutangazwa mshindi,Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Bi Mariam kajala, ameahidi ushirikiano zaidi na kwamba atakitumikia Chama na jumuiya zake uadilifu mkubwa
Amewaomba wagombea wengine ambao kura hazikutosha kupata nafasi hiyo, kutokata tamaa na badala yake waendelee kushirikiana na Chama na jumuiya zake ili kuleta tija na ufanisi
Kwa upande wake Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Shinyanga Mjini Bi Rehema Nhamanilo amesema baada ya Uchaguzi huo mdogo wajumbe wote wa jumuiya hiyo wanapaswa kuvunja makundi yaliyokuwepo ili kuendelea na majukumu ya kawaida katika kukijenga na kukiimarisha Chama na jumuiya zake zote
Naye kaimu katibu wa UWT Wilaya ya Shinyanga Mjini Naibu katalambula ambaye ni katibu wa UVCCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, amewapongeza wajumbe wa Mkutano huo pamoja na viongozi wote walioshiriki katika Uchaguzi huo mdogo,ambapo amesema demokrasia imechukua nafasi yake,kwa kuwa Uchaguzi umefanyika katika mazingira ya uwazi,usawa na haki,huku akisisitiza kuhusu wajibu wa kuendelea kushirikiana
Uchaguzi huo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa CCM Wilaya ya Shinyanga mjini,pamoja na wajumbe wa Mkutano huo lakini pia ulihudhuriwa na viongozi mbali mbali wa serikali,Chama na jumuiya akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Johari Samizi,Mwenyekiti wa UWT Mkoa Bi Grace Samwel Bizulu, katibu wa UWT Mkoa wa Shinyanga Asha kitandala, na Mary Mpazi Mjumbe wa Baraza la UWT Mkoa.