JAJI MFAWIDHI WA MAHAKAMA KUU KANDA YA SHINYANGA AWATAKA WANANCHI KUTUMIA MFUMO WA TEHAMA



Na Mapuli Kitina Misalaba

Jaji Mfawidhi wa mahakama kuu kanda ya Shinyanga (inajumuisha Mikoa miwili Shinyanga na Simiyu) Frank Habibu Mahimbali amewataka wananchi kutumia mfumo wa TEHAMA katika kufungua mashauri ili kuondoa malalamiko yanayosababishwa na ucheleweshaji wa kesi   mahakamani.

Ametoa wito huo  Alhamis Februari mos kwenye kilele cha maadhimisho ya wiki na siku ya sheria yaliyofanyika katika viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Shinyanga  wakati akizungumzia umuhimu wa mfumo jumuishi katika uendeshaji wa haki jinai ambapo amewataka wananchi kuwa tayari kupenda kutumia TEHAMA ili kupata taarifa zao kwa wakati juu ya hatua mbalimbali za mashauri.

Amesema Mahakama hiyo imeporesha mfumo wa TEHAMA ili kuendelea kutekeleza kwa vitendo dira ya utoaji haki kwa wakati kwa watu wote huku akisisitiza kutumia mfumo huo ili kuepukana na changamoto ndogo ndogo zilizokuwa zikiwakabili baadhi ya wananchi.

“Mifumo hii iko wazi na inapitika kwa kila mwananchi na kila mdau, mfumo huu umesaidia mambo yafuatayo usajili wa mashauri kwa njia ya mtandao madali popote na muda wowote siyo lazima ufika hapa Mahakamani lakini pia imetuwezesha upangaji wa mashauri kwa majaji na mahakimu kwa (Kidgitali) lakini uandishi wa hukumu na mienendo ya mashauri moja kwa moja kwenye mfumo tofauti na ilivyokuwa awal, vituo mbalimbali vya Mahakama kusomana na mifumo ya wadau muhimu wa Mahakama kama vile NIDA”.

“Faida nyingine ni kuweka nyaraka katika mfumo digit mfumo huu unasaidia Mahakama na wadau kusahau atha za upotevu wa nyaraka unaochangia na ucheleweshaji wa mashauri pia mfumo huu umesaidia sana mashahidi kuweza kusikilizwa popote alipo pasipo kupata atha ya kusafiri kufika Mahakamani nah ii inaokoa sana gharama za fedha muda na kurahisisha usikilizwaji wa mashauri, mfumo huu pia unawezesha wadau wa Mahakama kupata nyaraka mbalimbali kama vile hukumu uamuzi na sheria kwa njia ya elekronik ”.amesema Jaji mfadhi Frank

Jaji Mfawidhi wa mahakama kuu kanda ya Shinyanga Frank Habibu Mahimbali ametumia nafasi hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji nzuri wa TEHAMA nchini huku akimshukuru jaji Mkuu wa Tanzania profesa Ibrahim Juma kwa kuendelea kusimamia maboresha ya haki jinai na matumizi ya TEHAMA kwenye Mahakama.

Mahimbali   amewashukuru wananchi kwa ushiriki wao katika maadhimisho ya wiki ya sheria huku akiwataka kutumia vyema elimu waliyoipata katika maonyesho ya wiki ya sheria kwani  ni chachu ya kuleta mabadiliko chanya katika jamii .

Amesema ni muhimu kutumia kutumia elimu hiyo ikiwemo elimu ya masuala ya kisheria, kuleta mabadiliko  chanya katika mtindo wa maisha ya kila siku kisheria na kijamii.

Pamoja ma mambo mengine Jaji mahimbali amewataka watumishi wa mahakama kanda ya Shinyanga kufanyakazi kwa kuzingatia misingi ya sheria na kanuni zilizopo pamoja na kuwahudumia wananchi kwa weledi na uadilifu.

Solomon Lwenge kutoka ofisi ya wakili mkuu wa serikali kanda ya Shinyanga pamoja na mambo mengine amewasihi wadau wa haki jinai kuendelea kushirikiana katika kutoa elimu kwa umma kuhusu uzingatiaji wa utekelezaji wa sheria zinazohusu haki jinai kwa ustawi wa wa Taifa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme amesema serikali itaendelea kushirikiana na muhimili wa Mahakama kwa kuweka na kuboresha mazingira wezeshi  na salama ili kurahisisha upatikanaji  wa haki kwa wakati.

Maadhimisho ya wiki ya sheria yalifunguliwa rasmi Januari 24 ambapo kilele chake kimefikia hii leo February Mosi mwaka huu 2024 ambapo kaulimbiu ya Mwaka huu inasema “Umuhimu wa dhana ya haki kwa ustawi wa Taifa: nafasi ya Mahakama na wadau katika kuboresha mfumo jumuishi kwa haki jinai”.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Shinyanga wakiwemo wakuu wa vyombo vya ulizi na usalama huku taasisi mbalimbali ikiwemo Radio Faraja FM na Misalaba Media zikipewa vyeti kama sehemu ya kutambua mchango wao katika Mahakama ya kanda ya Shinyanga.Jaji Mfawidhi wa mahakama kuu kanda ya Shinyanga Frank Habibu Mahimbali akizungumza kwenye kilele hicho.Solomon Lwenge kutoka ofisi ya wakili mkuu wa serikali kanda ya Shinyanga akizungumza kwenye kilele hicho.
Burudani ikiendelea


Picha ya pamoja.

 

JAJI MFAWIDHI AKITAJA TAKWIMU ZA MASHAURI

This is received, thanks for your comments, will come back to you

Previous Post Next Post