VIONGOZI WA GIRL GUIDE WAANZA UTEKELEZAJI RASMI WA KAMPENI MKOANI SHINYANGA KUWAWEZESHA WASICHANA NA WANAWAKE KUFIKIA MALENGO YAO

 

Na Mapuli Kitina Misalaba

Chama cha Girl Guide kimezindua rasmi kampeni maalum Mkoani Shinyanga  inayolenga kuwawezesaha wasichana na wanawake kujiamini na kujithamini katika maisha yao ya kila siku.

Uzinduzi wa kampeni hiyo umefanyika katika shule ya msingi Buhangija Manispaa ya Shinyanga na kuhudhuriwa na baadhi ya wawakilishi kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Rwanda, Tanzania, Bangladesh, Zimbabwe pamoja na Madagascar.

Msimamizi wa miradi ya Girl Guide kutoka makao makuu, Valentina Gonza amesema chama hicho kipo nchi zaidi ya 52 Duniani ambapo pia amesema mpaka sasa zaidi ya wanachama milioni kumi wasichana na wanawake wamejiunga na chama hicho.

Gonze amesema Girl Guide ni chama cha kujitolea ambacho hakifungamani na dini wala vyama vya siasa huku akitaja malengo ya chama hicho ikiwemo kuwawezesha wasichana na wanawake kufikia ndoto zao.

 “Girls Guide ni chama cha kujitolea ambacho hakifungamani na dini yoyote kwahiyo unaweza ukawa mkristo, unaweza ukawa mwislamu na  unaweza ukawa mpagani  lakini pia chama hichi hakifungamani na vyama vyovyote vya siasa kwahiyo mtu yoyote anaweza akawa mwanachama kutoka sehemu yoyote, lakini pia ni chama ambacho hakichagui kazi au taaluma unaweza ukawa mwalimu, unaweza ukawa mwanafunzi, unaweza ukawa daktari, unaweza ukawa nesi, unaweza ukawa mjasiliamali unaweza ukawa mkulima kwahiyo ni chama ambacho mtu yoyote anaweza kujiunga”.

“Chama hiki kimejikita zaidi kuwajengea uwezo watoto wa kike na wanawake waweze kujitegemea, kujiamini, kuwa wazalendo na kuwawezesha waweze kufikia ndoto zao kwenye maisha yao kwa kupitia mafunzo ambayo yanatolewa na Girls Guide na mafunzo haya yapo kuanzia umri mdogo wanachama wetu ni kuanzia umri wa Miaka sita (6) na haya mafunzo yamegawanyika kulingana na umri husika kwahiyo watoto wenye umri kuanzia Miaka sita (6) hadi tisa (9) wanamafunzo yao maalum ambayo yanaendana na mahitaji ya huo umri”.

“Pia kuanzia umri wa Miaka kumi (10) hadi kumi na mbili (12) wanamafunzo yao maalum kwahiyo kila kundi lika linamafunzo maalum ambavyo yameshaandaliwa kwa ajili ya kuwasaidia wasichana”.

“Girls Guide ni chama ambacho kipo nchi zaidi ya 52 Duniani na kuna wanachama zaidi ya Milioni kumi wanawake na wasichama katika nchi mbalimbali ikiwemo Kenya, Uganda, Rwanda, Tanzania, Bangladesh, Zimbabwe, Madagascar na nchi zingine za afrika na Duniani kwahiyo tunapokuwa na huu umoja wetu inatufanya tuweze kujifunza vitu mbalimbali kujifunza tamaduni za wenzetu kujifunza jinsia gani wenzetu wanapambana na changamoto ambazo wasichana na wanawake zinawakabili kama vile masuala ya ukatili wa kijinsia pamoja na elimu ya utunzaji wa mazingira kwahiyo kwenye Girls Guide tunawajengea watoto wa kike uwezo wa kuwa na mifumo ambayo itatufanya sisi kuwa salama zaidi”.amesema Gonze

Ametumia nafasi hiyo kuwaomba wasichana na wanawake kujitokeza ili kujiunga na  Girl Guide na kwamba waweze kunufaika na fursa zinazojitokeza kupitia chama hicho.

Kampeni hiyo pia imelenga kutoa elimu katika jamii, kuachana na dhana potofu ambazo zimekuwa zikihusishwa kwa watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali ili jamii kutambua na kuthamini mchango wa watu wenye ulemavu na kwamba waweze kutoa fursa zawa na watu wengine.

Kwa upande wake mkufunzi wa chama cha Girl Guide Mkoa wa Shinyanga Veronica Marwa amesema matarajio ya kampeni hiyo kwa Mkoa wa Shinyanga ni kuwafikia wasichana elfu tatu (3000) kuanzia Julai 2 hadi Julai 6 Mwaka huu 2024 katika shule za msingi, sekondari na vyuo na kwamba zoezi hilo ni endelevu.

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Buhangija wameshukuru kwa elimu hiyo huku wakiahidi kushiriki kikamilifu katika kampeni za Girl Guige ili kufikia malengo yao.

Chama cha Girl Guide ni chama  kinachompa kila mtu uhuru na nafasi ya kuzungumza na kwamba kinaendesha mafunzo mbalimbali yakiwemo mafunzo ya hedhi salama, mafunzo ya kuwawezesha wasichama na wanawake kujiamini na kujithamini, kuheshimiana na kuepukana na mila potofu zilizopo kwenye jamii.

 


 

This is received, thanks for your comments, will come back to you

Previous Post Next Post